2.1
Watu wengi huona vipawa vyao na ujuzi wao kama tu njia ya maisha ya kawaida ya kujipatia mkate wa kila siku. Kutumia ujuzi wetu kujipatia maisha mazuri, kwa ajili ya familia zetu na kuishi maisha bora ni lengo la kawaida. Hakuna kitu kibaya na kusudi hili. Swali ni kama tumetengenezwa tu kwa ajili ya kufurahia maisha yetu au kwa ajili ya kusudi kubwa zaidi. Je, maarifa na ujuzi wetu ni kwa ajili ya kujipatia kipato au ni kwa ajili ya ibada?