Kundi la watu: Wabaka
Watu wa kabila la Wabaka wa kusini-mashariki mwa KamerunI ndio kundi kubwa zaidi kati la Mbilikimo kadhaa waliotawanyika kote Afrika ya Kati. Mbilikimo wana kimo kidogo, likiwa na wanaume watu wazima wasiozidi sentimita 155.
Wabaka wanaabudu roho ya msitu iitwayo Jengi (pia inajulikana kama Djengui au Ejengi). Wengi wanaishi katika kambi ndogo au vijiji vilivyotawanyika katika misitu ya bonde la Mto Kongo. Wao huwa wawindaji-wakusanyaji, kukusanya chakula chao cha kila siku kutoka kwa wanyama na mimea katika msitu wa mvua. Miti inapovunwa na wanyama kusumbuliwa, hali inazidi kuwa ngumu zaidi kutunza familia zao. Wengine wameanza kupanda mashamba na kufanya kazi kwa makabila jirani ya wakulima, lakini malipo ni kidogo.
Wabaka wanaona umaskini wao na kudharauliwa na wengine kama ushahidi wa uduni wao. Makabila mengine yanawapa hadhi ya chini kutokana na kimo na mtindo wao wa maisha. Walakini, wanaheshimu “kiroho” chao na uhusiano wao na uumbaji, wanakuja kwao kwa ajili ya kupata dawa.
Baadhi ya wamishenari kutoka World Team wamekuwa miongoni mwa Wabaka kwa zaidi ya miaka 16, wakijifunza lugha yao na kufanya uinjilisti na uanafunzi. Wanatoa mafunzo kwa wachungaji na viongozi, wakiwatia moyo kutumia utamaduni na ujuzi wao kufanya maisha bora na kanisa lenye nguvu zaidi kwa watu wao. Viongozi wachache wa makanisa mara nyingi hufanya kazi kwa wakulima wa jirani, zikiwaondoa kwenye kazi zao za kanisa.
Maisha yao ya kuhamahama na maeneo ya mbali hufanya elimu rasmi kuwa ngumu. Wabaka wengi hutumia njia za masimulizi kurithisha mila na desturi zao. Shirika la kimisheni, SIL, limeunda seti ya hadithi 37 za Biblia kwa ajili ya uinjilisti na mafundisho.
Ingawa kuna makanisa madogo yanayokua, kambi nyingi na vijiji havina ushuhuda wa Injili wenye nguvu. John Paul Gouffo, Mkameruni na Christian Missionary Fellowship International (CMFI), ni mmoja wa wamisionari wa kwanza wa ndani kwa Wabaka.
Kwa Kifupi
- Wabaka wanaamini katika Mungu muumbaji, Komba, lakini wanamwona kuwa yuko mbali. Badala yake wanamfuata na kumwamini Jengi, roho wa msituni.
- Uwindaji na uvuvi ni muhimu kwa utamaduni wa Baka, nao huweka vijito vya maji ili kuvua samaki.
- Wabaka wengi wametingwa na shughuli nyingi sana kila siku za kuwasaidia kuishi maisha yao hata wasiweze kufikiria mambo ya kiroho.
Omba kwa ajili ya
- Kazi inayozaa matunda ya watafsiri wanaojifunza lugha ya Wabaka na kuitafsiri Biblia kwa lugha hiyo.
- Bwana kujibu maombi ya Wakristo wa kabila la Wabaka ili kujenga imani yao.
- Umoja na baraka kati ya makanisa na huduma mbalimbali zinazohusika na Wabaka, na kwa waumini wa Wabaka kufikia watu wao wenyewe.
Vyanzo: Wikipedia na wamishenari wa World Team