Matamanio ya Dhati kwa Mama
Bishop Mussa M. Magwesela
Miaka mingi iliyopita, Elkana Chubugu kutoka Ntaza, alimkiri Bwana kupitia Wamisheni na akakua katika Imani. Aliendelea kukua katika safari yake ya kutembea na Bwana Yesu Kristo akiwa Mwinjilisti na kiongozi wa Kanisa mlei katika Kijiji chake na vijiji jirani. Bwana aliiheshimu huduma yake. Miongoni mwa watu aliowaleta kwa Yesu Kristo kupitia ushuhuda wake ni Ganagana Mboje ambaye alimwamini Bwana Yesu akiwa na umri wa miaka 14. Kisa hiki ni kumhusu mtumishi huyu wa Mungu ambaye baadaye alikuwa mchungaji wa Africa Inland Mission.
Ganagana Mboje alikuwa mtu wa kwanza nyumbani kwao kumfahamu Bwana Yesu Kristo. Baba yake mzazi alifariki wakati akiwa kijana mdogo. Hali hii iliongeza majukumu mabegani mwake kwa ajili ya mama yake na Doto Masunga wadogo zake akiwa ni mzaliwa wa kwanza. Ingawa hakufanikiwa kusoma katika mfumo rasmi wa elimu nchini Tanzania, aliuelewa ujumbe wa injili aliousikia kupita kwa Elkana Chubugu. Watu wa Ntuzu si rahisi sana kuyapokea mambo ya Kristo kama ilivyo kwa mtu wa tabia ya asili, kwa maana kwao ni upuzi. Ganagana alikuja kuwa mfuasi na mwanafunzi mwaminifu wa Kristo kupitia mikono ya Elkana Chubugu.
Sakwe, kijiji cha Elkana na Ganagana, ni jirani na mji wa Bariadi. Ganagana aliondoka nyumbani kwenda Bariadi kutafuta kazi. Kazi pekee ambayo angeweza kuipata ilikuwa ni kusaga unga. Ganagana, kupitia kazi hiyo alitegemewa kuwahudumia mama yake, wadogo zake na familia yake yote mahitaji muhimu. Bwana alikuwa akifanya kazi ndani ya Ganagana kwa njia ambayo hapana mtu aliyeweza kufahamu. Moyo ulikuwa ukimwaka ndani yake. Alikuwa akiomba awe mhubiri wa Injili. Shauku yake ilikuwa ni kufahamu kuhubiri. Ni neno la kumshukuru Mungu kwa vile Roho alimwezesha, yeye mwenyewe alijifunza kusoma na kuandika.
Aliamua kuacha kazi yake mwaka 1983 akajiunga na Chuo cha Biblia, Majahida. “Doto, mtoto wako amefanya uamuzi mbaya.” Kama kawaida, ndugu na majirani walimcheka mama yake na Ganagana. “Uamuzi huu wa mwanao utaifanya familia yako yote iendelee kuwa maskini maisha yote.”

Doto Masunga
Kila toleo lina makala ambayo itakufundisha zaidi kuhusu umisheni, kukuarifu kuhusu kile wamisionari wanafanya shambani, na kukuchochea kuwa hodari katika imani yako. Unaweza kuona makala yote na kupakua masuala bila malipo kwenye tovuti yetu kwa Walimdhihaki mama mzazi. Ganagana alibeba wajibu mkubwa sana wa familia. Aliwajali na kuwahudumia mahitaji yao ya kila siku. Kwa sababu hiyo kuacha kazi kulikuwa na maana ya kukata vyanzo vyote vya uchumi kwake mwenyewe, kwa mama yake, na kwa ndugu zake. “Lazima nijifunze kuhubiri.” Ganagana alijitia moyo.
Muhula wake wa kwanza Majahida haukuwa rahisi. “Irudie kazi yako, mwanangu. Unayafanya maisha yangu yakose tumaini.” Doto, mama yake alisisitiza. Mama alijitahidi kumzuia Ganagana asisome masomo ya Biblia. Mwinjilisti Elkana Chubugu pamoja na baadhi ya waalimu walijaribu kadri ya uwezo wao kumtuliza mama yake. Haikuwa rahisi. Mama aliendelea kulia akiamini kwamba mtoto wake amefanya uamuzi mbaya. Ganagana hakurudi nyuma. Alipohitimu alibaki chuoni kutumika akiwa mwinjilisti, kusimamia mashine ya kusaga unga pamoja na kuwa dereva. Mungu alimheshimu. Mboje, kama alivyokuja kufahamika, alimwoa Ephron kwa njia ya pekee sana. Mama yake na ndugu zake walifurahia sana vile mambo yalikuja kubadilika. “Bwana asifiwe sana kuwongoza mwanangu kufanya uamuzi sahihi.” Mama yake alisema. “Ndugu pamoja na jirani zangu hawakunishauri vizuri.” Mama alifariki akiendelea kumsifu Mungu.
Mboje alijaliwa kuwa mhubiri mzuri. Roho aliibariki huduma yake ya Injili hata miongoni mwa Wamasai ambako alitumika kwa miaka 15. Ametumika kwa uaminifu vijijini, mijini na katika majiji ya Tanzania kwa takriban miaka 40. Andrea, jina lake la kubatizwa, alistaafu kazi za mchungaji ili ahubiri Injili.