fbpx Skip to content

AfriTwende

Kulitia moyo
Kanisa katika
ulimwengu wa umisheni

Kwa zaidi ya karne, waafrika wamejitoa kutumikia katika utume, kuwarudisha waliopotea kwa Yesu Kristo na kusimika makanisa. Lakini karne mbili zilizopita zilikuwa kama karne za mazoezi au kupasha moto tu katika bara la Afrika, ambapo sasa kanisa limeimarika vizuri na Roho Mtakatifu akiendelea kuwaita watenda kazi katika utume kwenye jamii yenye mwingiliano wa tamaduni.

Ili kuchochea moto wa harakati za kitume, AfriGO ilianzishwa mwaka wa 2016. Jarida hili la AfriGo linalotolewa kila baada ya robo mwaka linasherehekea historia hiyo huku ikilitia moyo kanisa kuongeza ushiriki wake katika mpango wa kitume wa Mungu duniani. Wakati Kanisa la Afrika likitoa uongozi mpya na watenda kazi kuitangaza injili, AfriGO ipo kuwasimulia, kuwapa taarifa juu ya maendeleo hayo, na kuwashirikisha taarifa ili kuwaunga mkono wachungaji na wafanyakazi waliowatuma.

Ombi letu ni kwamba sauti za waafrika zinazozungumza kupitia chapisho hili zitachochea kupeleka mbele harakati mpaka upendo na utukufu wake Mungu utakapotangazwa duniani kote.

Masuala yaliyopita

Boti iliyo mbali ni simulizi ya kubuni ya Max, kijana Mkenya wa mjini, ambaye alikuwa na vyote: kazi ya ndoto zake, rafiki wa karibu, na msichana anayetarajia kumwoa. Akiwa katikati ya shida, Max alikutana na kitu cha ajabu, pale alipokutana na mvuvi mmoja masikini aliyekuwa Mwislamu, jina lake ni Yusuf. Maisha yote na mtazamo mzima wa Max ulitatizwa na kutiwa changamoto alipotambua Kuwa Yusuf na watu wake hawana na kanisa na hakuna hata shahidi wa mkristo wa kuwashuhudia. Baada ya kupata muda wa kupumzika, alimtembelea mjomba mzee mwenye hekima na alimshirikisha jinsi alivyoguswa na habari za Yusuf na watu wake, na katika mchakato huu, Max alitambua kuwa Mungu alikuwa akimwita ili awe mmisionari.