fbpx Skip to content

Wana na Mabinti Wa Afrika: inukeni na mumwombe bwana wa mavuno

By Jacob Igba

Kwa maana tokea maawio ya jua hata machweo yake jina langu ni kuu katika Mataifa; na katika kila mahali unatolewa uvumba na dhabihu safi kwa jina langu; maana jina langu ni kuu katika Mataifa. (Mal 1:11)

Leo shamba la umisheni limekuwa ndiyo nguvu ya umisheni! Kanisa katika Afrika linachukua mahali pake katika kuendeleza dhima ya Mungu katika ulimwengu wa umisheni. Lakini kwa mujibu wa Yesu katika Luka 10, hatua ya kwanza na muhimu ni kufanya hili: Kumwomba Bwana wa mavuno! Si pesa nyingi au tiketi ya safari ya ndege! Yeye ndiye anayeita watenda kazi wapya na kuwaamuru kuungana naye kwa kuomba ili atume watenda kazi zaidi. Wengi wamekuja kutambua wito wao kwa Mungu baada ya wakristo wengine kuomba kwa ajili yao.

Kama Samweli Zwemer alivyowahi kusema, “Historia ya umisheni ni historia ya maombi yaliyojibiwa. Ni ufunguo kwa ajili ya tatizo lote la umisheni. Njia zingine zote za kibinadamu ni kitu cha pili.” Zwemer alikuwa ni mmishonari wa kwanza wa muda mrefu aliyefanya kazi katika ulimwengu wa kiarabu, akitumika kutoka mwaka 1891 hadi 1929, na alipewa jina la utani kama mtume wa Uislamu. Katika hekima ya Mungu inayopita zote, alibuni shughuli ya umisheni kuwa ndiyo moja ya kitu pekee cha kumtegemea Mungu katika maombi. Mungu hukamilisha makusudi yake katika majibu kwa maombi ya watu wake.

Kanisa la Afrika linajulikana kama kanisa linaloomba. Linamiliki rasilimali hii muhimu inayohitajika kwa maendeleo ya Umisheni wa Mungu duniani. Lakini rasilimali hii inahitaji kuelekezwa zaidi  Mungu anawaita wengine kwenda na wengine kukaa, lakini anatuita sisi sote kuomba. Anawategemea wale ambao wamebaki kuhubiri mahali walipo, wakiwafanya watu kuwa wanafunzi, wakiwatuma wanafunzi na kuomba. Wale waliotumwa kwenda mbali wakati wote wanahitaji kundi la watumaji waliojitoa kusimama nao katika maombi na kuwategemeza kwa msaada wa kifedha. Kupitia maombi ya kimkakati na yasiyokoma, (Luka 11:1- 10), viongozi, makanisa, wana na binti wa Afrika ambao wamo ndani ya Kristo wanaweza kuinuka. Waweza kushikamana fursa hii na heshima hii ya kuungana na Mungu katika haja hii ya heshima kwa ajili ya kumfanyia ibada kwa “kusafiri kwa magoti yetu.” Nchi zinaweza kubadilika kwa sababu ya maombi yetu (angalia mfano kwenye pembezoni).

Mmishonari Luka Herrin, Mkurugenzi wa kimataifa wa Africa Inland Mission (AIM) aliwahi kushauri, “Ombeni ili Bwana atume watenda kazi zaidi, ombeni ili Bwana atume watenda kazi kutoka miongoni mwenu (kanisa lako la mahali, kikundi cha usharika ) na ombeni ili Bwana akutume wewe.” Hapa chini ni baadhi ya maswali ya kutafakari:

  • Unafanya nini katika muktadha wako kuomba kwa ajili ya kazi za umisheni na wamishonari?
  • Kanisa lako linafanya nini katika kuomba kwa ajili ya umisheni na wamishonari?
  • Ni hatua gani mahususi unaweza kuchukua kuongeza maombi na kuunga mkono kwa wakristo kutumwa kwa waliopotea?

Maombi Yaliyojibiwa   “Nilitumikia miaka minne katika Afrika ya Kaskazini pamoja na familia yangu kama mmishonari… Nchi yote ilikuwa na waislamu wengi, huku kukiwa na pengo kubwa kati ya matajiri na maskini. Polisi mafisadi waliwasumbua madereva wa teksi. Hali ya usafi haikuwepo kabisa kutokana na uhaba wa maji. Jumapili ilikuwa ni siku ya kufanya kazi kitaifa. Hali hiyo ilihitaji hatua ya haraka. Kwa hiyo, viongozi wa kikristo waliandaa orodha ndefu ya maombi ikijumuisha karibu kila hitaji la kitaifa na kukusanya watu kutoka makanisa machache ya kiinjili katika mji mkuu ili kuanza siku 40 za kufunga na kuomba kwa ajili ya vita ya kiroho.” Matokeo yalikuwa ya kushangaza. Juma lile lile tulipoanza kuomba kuhusu ufisadi wa polisi, madereva wa teksi walianza mgomo. Katika uchunguzi, serikali iliagiza polisi wote waondolewe barabarani na vizuizi vyote viondolewe ili kutoa nafuu kwa kila mtu. Pia, katika hilo juma ambalo tulikuwa tunaomba kuhusu hali ya usafi katika mji, magari makubwa ya kuzoa taka kama 50 yaliyotolewa msaada na nchi ya Israeli yalianza kuzunguka na kuzoa taka.  .”     – J.F.K Mensah wa Ghana

4.4 Jacob Igba

Dk. Jacob Igba anatumika kama mratibu wa uhamasishaji kwa eneo la Afrika Kusini kwa Africa Inland Mission (AIM). Yeye anatoka Nigeria, uzoefu wake ni pamoja na huduma kwa vyuo vikuu, upandaji makanisa miongoni mwa mataifa ya Kiislamu ya Nigeria kaskazini, na kufundisha Agano Jipya, elimu juu ya Kristo, elimu juu ya Mungu, na umisheni. Jacob na mkewe Juliet wana watoto wawili wa kiume.

share
share
Instagram
contact us
contact us
contact us