Skip to content

Tuliomba kwa ajili ya uponyaji na nikaponywa! – nyakati za wamishenari

Mwaka 1977 nikiwa shule ya msingi nilikuwa na matatizo ya macho, nilikuwa nikihangaika kuona. Nilipelekwa hospitalini, lakini daktari aliponichunguza, aliniambia kwamba hakuweza kupata chanzo cha tatizo la kutokuona kwangu kitabibu. Jioni yake nilikutana na Mwinjilisti wa kanisa la Afrika Inland Church (AIC) aitwaye Samweli, ambaye alinialika kwenye mkutano wa injili. Mwishoni mwa mkutano nilienda mbele kwa ajili ya maombi, tukaomba kwa ajili ya uponyaji na nikaponywa! Nikamwamini Bwana Yesu na nikaamua kwamba nitajitoa maisha yangu katika huduma yake.
Nilikaribishwa na wamishenari wa AIM wa Kanisa la Africa Inland Church kufanya kazi katika Taasisi ya Biblia na Huduma hapa Tanzania (Institute of Bible and Ministry) katika nafasi ya uangalizi (caretaker) mwaka wa 2016, ingawa nilikuwa napafahamu mahali hapo kabla. Fursa ya kufanya kazi mahali hapa ni kudhihirika kwa neema ya Mungu, na siwezi kujisifu kuhusu hilo! Namshukuru Mungu kuwa sasa mimi ni sehemu ya kazi yake hapa Sanga Sanga.
Pia ninaongoza kanisa lililoko Kiloka (takribani maili 30 kutoka Morogoro). Eneo hili lina Waislamu wengi. Watu wanaponiuliza kwa nini ninajisumbua na upandaji kanisa, ninacho waeleza tu ni kwamba ni mpango wa Mungu. Yesu, katika Mathayo 28:19, aliwaambia wanafunzi wake waende kuhubiri injili, kwa hiyo ilinibidi kufanya hivyo! Pia tumeamriwa kuwa nuru katikati ya giza.
– Francis Manungu
Soma zaidi hadithi hii (kwa Kingereza) kwenye https://eu.aimint.org/why-bother-church-planting/
share
share
Instagram
contact us
contact us
contact us