“Mbwa mwitu mmoja mweusi ” – nyakati za wamishenari

“Siku moja Watu walipanga jambo ambalo hatukulijua, mbwa mwitu mmoja mweusi aliingia ndani ya nyumba yetu na akakaa. Hatukujua asili ya yule mbwa. Tulimpatia jina la Ginger (Tangawizi). Mbwa yule alikaa na sisi kwa muda mrefu. Ikawafanya watu waogope kuikaribia nyumba yetu kwani mbwa angewafukuza. Ilikuwa kana kwamba mbwa anaweza kusoma mawazo ya watu. Hakumung’ata mtu yeyote lakini alihakikisha anatulinda. Asubuhi tukiwa tunaenda ofisini, mida ya saa 2, mbwa alikuwa anatusindikiza na kurudi.
Siku moja, mbwa alipotea, na paka akaja kuchukua nafasi yake. Alikuwa paka wa mwituni kama yule mbwa. Hakumudhuru hata mtu yeyote kati yetu lakini alikuwa anatufuata ofisini. Hatukuwahi kufikiria kuwa anaweza kuwa malaika. Mungu anawezaje kumfanya paka awe kama malaika? Kama watu wangetuua, pia hata maono yetu yangekufa. Baada ya kutafakari juu ya hili, ilionekana dhahiri ya kuwa mbwa na paka hawakuwa wa kawaida. Na baada ya muda, paka alitoweka. Haya yalitokea baada ya muda mfupi kabla hatujaondoka Zaria.”
Kutoka katika kitabu cha CAPRO: “From Africa to the World: hadithi ya CAPRO” na Festus Ndukwe, iliyochapishwa 2019.