“Kuwafikia watoto” – nyakati za wamishenari
Laurent Charles Mgaya, mmishenari wa Rivers of Life Ministries, Dar es Salaam, TanzaniaNilikulia katika familia ya Kikristo mpakani mwa Zambia na Tanzania, na nilijifunza njia za Bwana tangu nikiwa mdogo. Mama yangu alikuwa mwalimu wa Shule ya Jumapili (Sunday School), nami nilikuwa nikifuatana naye alipokuwa akienda kufundisha.
Nilipokuwa na miaka tisa, baba yangu alifariki. Mwaka huohuo, nilianza kufundisha kanisani pamoja na mama yangu. Alitufundisha nidhamu zote za maisha ya Kikristo, ikiwa ni pamoja na kufunga na kuomba.
Mwaka 2017, nilikutana na mmishenari wa CAPRO ambaye alinifundisha kuhusu makundi ya watu ambao hawajafikiwa. Nilianza kwenda naye katika maeneo ya huduma ya umisheni, nikijifunza kile alichokuwa akifanya. Nikiwa nimehamasishwa na huduma yake, nilijiunga na Nigeria Intercultural School of Mission kwa mafunzo ya umishenari.
Niliporudi nyumbani baada ya mafunzo, nilianza huduma ya kuwafikia watoto jijini Dar es Salaam. Tunawafikia watoto kwa upendo wa Kristo na kuwafundisha Neno la Mungu, nao watoto huwafikia familia zao. Takribani robo tatu ya watoto hao wamewafikia wazazi wao, na sasa wazazi wengi wameanza kujiunga na kanisa.
Soma simulizi kamili hapa: