Skip to content

“Kutoka kuwa wakimbizi hadi wamishenari” – hadithi za kimishenari

Mwaka 2005, nilikuwa mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo nikiishi katika kambi ya wakimbizi huko Nampula, Msumbiji. Niliomba kila mara kwamba Mungu afanye muujiza: aniruhusu kutoka kambini ili niweze kumtumikia popote. Hatimaye, mmishenari mmoja alinibariki kwa kunipatia fedha za kusoma katika Chuo cha Theolojia cha Scott nchini Kenya, ambako nilisomea Theolojia na Masomo ya Tamaduni Mbalimbali.
Mwaka 2007, niliondoka Kambi ya Wakimbizi ya Maratane kuelekea Congo ili kupata pasipoti. Bwana alitoa miujiza kwa kutupatia fedha kupitia marafiki. Tulifunga ndoa na wiki moja baadaye tukasafiri kwenda Kenya. Kabla ya kuhitimu, mimi na Rachel tulitumia miezi sita tukimwomba Mungu atuonyeshe mwelekeo wa huduma. Mungu alijibu maombi yetu kupitia rafiki yetu kutoka Tanzania aliyetuambia kuwa amepewa jukumu la kuongoza timu kupitia shirika la Africa Inland Mission (AIM) na Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT).
Tulikubali mwaliko wake wa kufanya kazi katika wilaya ya Kondoa, eneo la vijijini lenye Waislamu wengi, kwa kipindi cha miaka miwili na nusu. Timu yetu ilinichagua kuwa mratibu wa maombi. Kila Jumatano kuanzia saa 11 jioni hadi saa 3 usiku, tulikuwa tukiomba kwa ajili ya watu kwa kuwataja majina yao.
Mungu alijibu maombi yetu kwa kufungua milango ya kushiriki injili na wale tuliokuwa tukiwaombea. Baadaye, tuliitwa kufanya kazi katika kanisa moja jijini Nairobi, Kenya, lakini hatukupata vibali vya kazi. Badala yake, Mungu alituongoza kuwa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Africa International University (AIU). Nilikamilisha shahada ya Uzamili katika Misheni (nikijikita kwenye Uislamu), na Rachel alikamilisha shahada ya Uzamili katika Maendeleo ya Mtoto na Masomo ya Familia.
Leo hii, tunahudumu kama wamishenari kupitia shirika la AIM (Africa Inland Mission).
share
share
Instagram
contact us
contact us
contact us