“Hata wanawake waliruhusiwa kucheza!”-nyakati za wamishenari

Kwa hiyo, Mabalozi walianza mafunzo kwa ngazi ya juu ya uongozi wa kanisa, wakiwakumbusha ushauri wa Paulo katika 1 Wakorintho 9:22b: “Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.” Ili kuwafikia vijana ambao walikuwa hawaji kanisani, lazima watu wawe watu wa michezo ili waweze kuwavutia vijana ambao wapenda michezo. Walionyesha mfano wa huduma ya mwili kwa viongozi, na kwa ruhusa yao walianza kidogo kidogo, waliomba kanisa litume watu/vijana wao walio wazuri kwenye michezo ili kwa namna hiyo waifikie jamii. Hatimaye, hata wanawake waliruhusiwa kujiunga – na kuvaa suruali!
Mabalozi walisisitiza Kandanda (Mpira wa miguu), Imani na Kesho iliyo bora, na lengo la kila mkusanyiko ni Kujifunza Biblia pamoja na michezo na uchezaji. Watoto wadogo wanahimizwa kukariri Maandiko (Mistari). Sasa, ni moja ya programu kubwa Afrika!
Jean Paul Seneza, Mkurugenzi wa Ambassadors Football Africa