fbpx Skip to content

Kupitia Safari Fupi Za Kimisheni

Tafakari kundi la vijana likisafiri pamoja kwenye mwambao wa pwani ya kaskazini ya Msumbiji. Wanatoka nchi ya Lesotho, Botswana, na Kenya. Je, hawa ni watalii? Au wanafunzi wa Chuo Kikuu kwa kazi maalum? Hapana. Hawa ni vijana wamishonari wakiwa kwenye safari fupi ya majuma manne.

Watu ambao bado hawajafikiwa, jamii ya Macua Nahara, wana imani tu ya kindugu ya kiislamu na wana mashaka sana na watu kutoka nje ya maeneo yao. Kiwango cha elimu yao ni kidogo, asilimia 20 tu ya wanaume na asilimia tano ya wanawake ndiyo wanaweza kusoma na kuandika. Wanakataa kabisa Injili.

Mwezi wa Oktoba mwaka 2019, wamishonari watano ambao hawakuwa na uzoefu wa kazi za umisheni lakini wenye moyo mkuu wa kufanya kazi za kimishonari walifika katika hali hii. Baadhi yao walikuwa na ndoto ya kuwa wamishonari kwa miaka mingi. Wengine, kama Rosy kutoka Lesotho alisikia juu ya safari akiwa kanisani: “Nilihamasika kutokana na habari nilizozisikia na kwamba nilitaka kutoka nje na kuona jinsi ambavyo nami ningeweza kutumika.” Kiongozi wa safari August Basson ni mishonari mwenye uzoefu na ambaye ndoto yake imekuwa ni kuwaandaa wamishonari wa kiafrika. Mwaka jana, aliongoza timu ya vijana wa kiume kwenda kusini mwa Tanzania, na matokeo yake – timu ya huduma ya mavuno ilizaliwa.

Kikundi kilisafiri kwenda kwenye kijiji kilichoko Pwani, kikatengeneza nyumba ya matope na kukaa huko kwa muda wa juma moja. Walijifunza baadhi ya lugha za kienyeji, walifanya shughuli za vijana, waliongoza michezo, na walijifunza na kufundisha nyimbo. Walisaidia kukaa na watoto ili mmishonari mwenye uzoefu aweze kufundisha neno la Mungu na hata kutumia mashine za kufundishia sauti za lugha ili kusaidia kufundisha watu kusoma na kuandika.

Mmishonari Grant Franke kutoka Afrika ya Kusini na familia yake wameishi na kufanya kazi katika jamii ya Macua Nahara kwa miaka minane. Alifundisha timu yake baadhi ya semi za lugha ya Macua Nahara kila siku na walizunguka katika kijiji wakifanyia mazoezi kile walichofundishwa, wakiwaalika watu kuja kwenye mafundisho ya Biblia na pia kupata masomo ya kilimo na kujifunza kusoma. Grant alisema mahudhurio yalipanda mpaka kufikia asilimia 1000 na hata wanawake ambao ni nadra kujitokeza katika jamii hiyo nao walikuja.

Vijana wadogo wa kike katika kijiji walifanya kazi zaidi na timu ya mavuno ya wanawake. Wasichana hawa wanaishi katika mazingira ambayo ni hatari sana, na kwa hiyo walijisikia salama kuwa na timu yetu. Walipowaaga, wengi wa wasichana hao walisononeka.

Grant alisema: “Ni jambo lenye matokeo mazuri sana pale Waafrika wanapokuwa wamishonari kwa Afrika. Wameweza kuaminiwa zaidi ndani ya juma moja kuliko miaka minne niliyotumia mimi”. Anasema mara kwa mara amekuwa akiulizwa kuwa lini tena timu itarudi kuwatembelea.

Kwa huzuni, kwa kawaida huwa kuna matokeo kidogo ya muda mrefu katika jamii zilizotembelewa na timu za kimisheni za muda mfupi. Wanajenga kuaminiana au kutatua matatizo ya kijamii, lakini matokeo ya muda mrefu huja katika maisha ya timu na Makanisa yao. Mwana-timu ya mavuno, Lerato alisema: “Nimekuwa nikitafakari kufanya kazi ya umishonari- sasa nina uhakika nataka kuwa mishonari wakati wote”.

Wamishionari wengi wenye uzoefu wanasema safari fupi zilisaidia kuthibitisha kuitwa kwao. Wale ambao hawawezi kwenda hugeuka kuwa watu wanaosaidia na kuwaombea wamishonari walioko kazini –kwenye shamba la mavuno. Safari fupi za kimisheni huhamasisha kanisa kuwategemeza kwa maombi na msaada wa pesa walio watuma. Safari fupi ni zana yenye matokeo mazuri kwa kuwaandaa watu kwenda, kutoa na kuomba kwa ajili ya makundi ya wamishonari duniani kote.

Je, ungetamani kuwa mmoja wa wana-timu wa umisheni wa muda mfupi? Wasiliana na August Basson kwa: august.basson@aimint.org Kujua zaidi kuhusu [Harvest Team]. Kuwaombea Macua Nahara, tembelea www.nahara.info Mtaalam wa masuala ya vyombo vya Habari Halley McNeill akifuatana na Timu ya Mavuno. Angalia safari yao ya kusisimua kwenye Facebook:  www.facebook.com/The-Harvest-
Africa-116173849768069/. Itakusisimua!

share
share
Instagram
contact us
contact us
contact us