fbpx Skip to content

Makundi ya Watu: Wazigua

Wazigua ni jamii ya watu wenye asili ya kibantu wanaoishi katika ukanda wa pwani ya kaskazini-masharikki mwa Tanzania. Lugha yao ni Kizigua, na pia wengi wao wanazungumza Kiswahili viziuri.

Baada ya kukimbia biashara ya utumwa huko mashariki, Wazigua waliweka makazi yao karibu na Dar es Salaam. Historia ya Wazigua ni ya zamani. Leo hii idadi yao ni kama 631,000 hivi. Nchini Tanzania Wazigua bado wanahesabika kama ni miongoni mwa makundi ya pembezoni, wakiwa bado ni jamii ya watu wenye kiwango kidogo cha elimu.

Dini yao kuu ni Uislamu ukiwa umechanganyika na mapokeo ya tamaduni za kuabudu mizimu au roho za mababu zao. Mara nyingi watoto wao hupelekwa kusoma elimu ya Kiislamu yaani madrasa. Idadi ya wakristo miongoni mwa Wazigua ni ndogo sana isiyozidi asilimia tisa.

Wazigua ni jamii yenye undugu wa karibu. Wanaishi pamoja katika vibanda vilivyokandikwa kwa matope na kuezekwa kwa nyasi na vilivyo kwenye kundi moja la pamoja. Maisha yao yanategemea ukulima mdogo na uvuvi. Kama ilivyo kwa miji mingi ya pwani ya Tanzania, zao lao kubwa la biashara ni mkonge na mazao makuu ya chakula ni mahindi na ufuta.

Wamisionari wamekuwa wakiwafikia Wazigua kwa miaka mingi. Katika mwaka 2017, Africa Inland Mission (AIM) ilianza kazi katika eneo jipya kwa mtazamo wa kuwahubiria Injili Wazigua na kuboresha maisha yao. Kazi ya kufasiri, kwa maana ya Agano Jipya na Filamu ya Yesu sasa zinapatikana katika lugha ya kizigua. Unaweza kujifunza zaidi: https://prayafrica.org/project/zigua-of-tanzania/

Mtazamo wa Haraka- Muhtasari

  • Wazigua walikimbia utumwa na kisha kuweka makazi yao katika pwani ya Tanzania. Idadi yao ni kama 631,000 hivi.
  • Dini yao kuu ni Uislamu, ukiwa umefungamanishwa na mila za asili na ibada za mababu zao. Wakristo ni kama asilimia tisa tu.
  • Ni moja ya makundi ya pembezoni wakiwa na kiwango cha juu cha kutojua kusoma na kuandika na ukosefu wa ajira.
  • Kazi ya kutafsiri mpaka sasa imetoa Agano Jipya na Filamu ya Yesu.

Omba

  • Kwamba kazi ya Injili inayoendelea izae matunda.
  • Wazigua wapate uhuru wa kweli katika Kristo kutoka kwenye dini za asili na ibada za mababu zao.
  • Kwamba watenda kazi waende maeneo ya Uzigua na kuishi huko, ili kuwahubiria injili kwa moyo, kwa maneno na kwa matendo.
  • Waamini wapya waweze kudumu katika imani na kuanza kuzifikia familia na jamii kubwa ya wazigua.
share
share
Instagram
contact us
contact us
contact us