Skip to content

“Nilifukuzwa nyumbani” – nyakati za wamishenari

Verissimo Francisco, mmishenari kwa Wakuvale nchini Angola
Nilizaliwa katika mji wa pwani kusini mwa Angola na nikakulia katika kanisa lililochanganya imani ya kiinjili na desturi za jadi za Kiafrika.
Nilipokuwa na umri wa miaka 17, nilijiunga na kikundi kilichoniongoza katika safari ya kumfuata Kristo. Lakini nilipowaambia wazazi wangu kuhusu uamuzi huo, walinifukuza nyumbani.
Marafiki walinipokea na kunipa mahali pa kuishi. Baada ya kumaliza shule, nilihisi Mungu akiniita kwenda kuwafikia wengine ili kuwapelekea Injili.
Shirika moja la umishenari lilitaka kunipokea katika huduma yao, lakini kwa kuwa sikuwa na vyeti vya kitaaluma, serikali haikuniruhusu kuhubiri. Hivyo nilijiunga na Instituto Superior De Theologica no Lubango (ISTEL), ambako nilipata shahada ya miaka minne ya theolojia na umishenari.
Kwa muda mrefu nilikuwa nikijua kwamba Mungu alikuwa akiniita kuwafikia Wakuvale, kundi la watu ambao hawajafikiwa na Injili. Mwalimu wangu wa ISTEL alitambua wito huo mapema, na shirika moja la umishenari lilipoomba shule ipendekeze mtu wa kujiunga na timu yao, alilipendekeza jina langu.
Kwa sasa nimehudumu kama mmishenari miongoni mwa Wakuvale kwa miaka mitatu. Pia nasafiri mara kwa mara kandokando ya mto ili kuandaa njia ya Injili miongoni mwa watu wa Thimba na Himba kusini mwa Angola.
Soma simulizi kamili kwa kiingereza hapa: