Mmishenari katika maeneo ya Sahel – nyakati za wamishenari

Mmishenari kutoka Malawi aliyeenda maeneo ya Sahel
Nilipokea wokovu baada ya kusikia mahubiri kutoka katika kitabu cha Yohana 3:16. Andiko hili rahisi lilinijia kwa namna mpya kabisa; ilikuwa kana kwamba nilikuwa nikilisikia kwa mara ya kwanza. Niliitikia mwito wa madhabahuni na nikampokea Kristo.
Baadaye, nilijiunga na World Mission Center (sasa inajulikana kama Blantyre School of Mission). Nilihisi wito thabiti wa kuwa mmishenari. Nilijifunza kwamba huu ulikuwa mpango wa Mungu na mzigo alioubeba kwaajili ya ulimwengu, nami nilitamani kuwa sehemu yake.
Mungu alinipa maono kwa ajili ya watu wa Twa nchini Burundi. Nilijiunga na CAPRO, na kutoka Malawi nikatumwa Kenya kwa mafunzo zaidi ya umishenari katika CAPRO School of Missions. Nilishiriki maono yangu kuhusu Burundi, na baada ya kuhitimu mwaka 2003, nilitumwa Togo kuhudumu kama mmishenari huku nikijifunza lugha ya Kifaransa.
Baadaye nilihudumu Burundi kwa miaka sita kama mmishenari chini ya CAPRO.
Nikiwa katika kipindi cha mapumziko, nilikutana na mmishenari mwenzangu wa CAPRO nchini Kenya. Tukapendana na kufunga ndoa. Tulihudumu Burundi na Kenya hadi mwaka 2020, Mungu alipotuelekeza kujiunga na huduma nyingine, Operation Mobilization (OM).
OM ilitutuma katika eneo la Sahel. Tunawafikia wenyeji kwa kutumia mbinu ya Discovery Bible Study (DBS). Tunazunguka katika jamii mbalimbali tukifanya matembezi ya maombi. Tunapokutana na mtu mmoja anayepokea ujumbe wetu, mara nyingi hutupeleka kwa familia yake, na hapo tunafanya nao mafundisho ya Biblia.
Soma simulizi kamili hapa:
https://afrigo.org/story_resources/missionary-profile-e-from-malawi/