“Vijana wanapaswa kwenda!” – nyakati za wamishenari

Nilipokea Injili nikiwa bado mdogo ambapo ilikuwa katika kambi ya Scripture Union. Sikujua mengi kuhusu umishenari hadi nilipokuwa chuoni.
Kabla ya kwenda kwenye safari yangu ya kwanza ya umishenari ya muda mfupi, niliogopa kwamba ningeenda Injili ingekataliwa. Nilipopata ujasiri na kwenda, hamasa na namna Injili ilivyopokelewa ilinifanya nitambue kwamba kutokwenda kwangu kungekuwa kosa kubwa sana.
Mwaka 2018, nilisikia kuhusu Excellent Youth Outreach (EYO) na nikajiandikisha nao. Mwaka 2019, nilifanya safari yangu ya kwanza ya umishenari wa kwenda kwenye tamaduni nyingine huko Uganda na baadaye Côte d’Ivoire, ambako nilikutana na mwanaume mmoja aliyekuwa amelewa. Alivutiwa nasi na kile tulichokuwa tukizungumza. Kama mkalimani wa kundi, nilimwambia, “Sisi ni wamishenari tuliokuja kukuambia kwamba Yesu anakupenda.” Alisema aliona maisha yake yameharibika na alihitaji tumsaidie.
Tangu wakati huo, nilitambua hitaji langu la kujihusisha kikamilifu katika kuhubiri Injili duniani kote, iwe karibu nami au mbali na nyumbani. Leo, mimi na timu yangu tunatumia shughuli za kawaida kama mashindano ya upishi, masomo ya Biblia kwa watoto, na programu nyingine kuwafikia watu.
Ninalitia moyo Kanisa barani Afrika lijihusishe na kazi ya umishenari, kwanza kwa maombi, kisha kwa kwenda. Vijana hasa wanapaswa kutiwa moyo kwenda. Wako wengi, na wana nguvu na muda.
Soma hadithi nzima kwa Kiingereza https://afrigo.org/story_resources/missionary-profile-olivia-acheampong/